SIMBA SC
AZAM FC
MABINGWA wa ligi kuu soka Tanzania
bara Simba na Mabingwa wa michuano ya kombe la Mapinduzi Azam FC kewsho
watakutana katika mchezo wa fainali wa michuano ya kombe la urafiki utakaopigwa
kwenye dimba la Amaan, visiwani Zanzibar .
Azam imetinga hatua hiyo baada ya kuikwanyua Super Falcon mabao
2-0 huku Simba ikikata tiketi hiyo baada ya kuifunga All Stars bao 1-0.
Mchezo huo wa fainali utakuwa wa pili kuzikutanisha timu
hizo katika michuano hiyo ambapo awali zilikutana katika hatua ya makundi na
kutoka sare tasa.