WAKATI Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (Tamisemi), Kassim Majaliwa, leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi
kwenye uzinduzi wa kipindi cha Simba Tv kitakachokuwa kikirushwa na kituo cha
runinga cha Clouds, mawaziri, wabunge na viongozi mbalimbali wa kiserikali
ambao ni mashabiki na wanachama wa Simba wakiongozwa pia watahudhuria.
Kama hiyo haitoshi uzinduzi huo pia utahudhuriwa na wadau mbalimbali wa timu hiyo na soka kwa ujumla pamoja na wanachana na wachezaji wa zamani wa timu hiyo.