mAJURA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
limewapongeza waandishi watatu wa habari za michezo kwa kushinda tuzo ya
uandishi bora ya EJAT inayotolewa na Baraza la Habari Tanzania
(MCT).
Waandishi hao walioshinda
katika kategori ya mpira wa miguu ni Imani Mani wa Daily News (magazeti),
Abdallah Majura wa 91.2 Sport FM (redio) na Anuary Mkama wa Mlimani Media
(televisheni).
TFF inawapongeza waandishi
hao kwa ushindi huo uliotokana na makala zao ambazo zina mchango katika
maendeleo ya mpira wa miguu, lakini pia ni changamoto kwa waandishi wengine
ambao hawakufanikiwa kushinda.
Vyombo vya habari vina nafasi
kubwa katika ustawi wa mpira wa miguu, kwani katika nchi nyingine vimefichua
rushwa katika mpira wa miguu. Ni matarajio yetu kuwa vyombo vya habari nchini
navyo vitakuwa mstari wa mbele katika kufichua na kupambana na rushwa katika
mpira wa miguu nchini.