MSANII wa muziki wa bongo
fleva Dogo Aslay anatarajiwa kuzindua
albamu, filamu pamoja na kitabu vikibatizwa kwa jina la ‘Naenda Kusema’ ,
uzinduzi utakaofanyika Juni 24 katika ukumbi wa Dar Live, jijini Dar es Salaam.
Meneja
wa kundi la TMK Wanaume Family Said Fella amesema leo kwamba maandalizi kwa
ajili ya uzinduzi huo yanakwenda vema ambapo msanii huyo yupo katika mazoezi
makali ya kujiandaa.
Alisema msanii huyo amepania
kutoa burudani ya aina yake ambayo itamfanya kila atakayehudhuria onyesho hilo kusuuzika na roho
yake hivyo amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi.
Alisema katika uzinduzi huo,
Dogo Aslay atasindikizwa na wasanii mbalimbali wakiwemo TMK Wanaume Family, Mkubwa na Wanawe, Ferooz,
Mwan Fa na Ize Man.