MAPRO HAWANA LOLOTE-MTIBWA SUGAR


 Kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime

KOCHA wa timu ya Mtibwa Sugar,Merky Mexime,amesema wachezaji wakimataifahawana nafasi katika kikosi chake. 
 Mexime alisema wachezaji wengi wa kigeni wanaokuja nchini hawana uwezo uanjani licha ya kukumbatiwa na klabu kubwa. 
 Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa,Taifa Star”,alisema wachezaji wazalendo wanamchango mkubwa katika klabu za soka. 
Alisema Tanzania ina wachezaji wazuri na wana uwezo mzuri,lakini hawapewi nafasi kima ilivyo wakimataifa wanaogeuka lulu. 
“Natamani hata wasije kucheza nchini,hawana lolote kulinganisha na wachezaji wetu ndio maana mtibwa hatusajili wachezaji wa kigeni.”alisema Mexime. 
Alisema klabu za Simba na Yanga zinapaswa kubadilika na kuwatumia wachezaji wazalendo ili kuongeza viwango vyao vya soka. 
Alisema wachezaji wa Tanzania wakitumika vyema wana nafasi kubwa ya kupata timu nje ya nchi. 
Mbali na Simba na  Yanga,Azam ambayo imekuwa tishio kwa vigogo hivyo ni miongoni mwa klabu zilizosajili wachezaji wa kimataifa . 
Yanga ina kipa yam Berko,Hamisi Kiiza na Haruna Niyonzima. 
   Simba ni Emmanuel Okwi,Felex Suzu na Azam ni Kipre Tchetche.
CHANZO:Gazeti la Uhuru

Post a Comment

Previous Post Next Post