TFF YAPONGEZA AMSHA AMSHA YA USAJILI


SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) limeeleza kufurahishwa na hamasa iliyoko katika usajili hapa nchini.
Hayo yalisemwa jana na Rais wa TFF, Leodger Tenga alipozungumza na wahariri wa michezo wa vyombo mbalimbali vya habari nchini.
Hata hivyo, Tenga alikosoa watu wasio wataalamu wa ufundi kuendesha zoezi hilo, badala ya makocha au kamati za ufundi.
Alisema walikubaliana kuruhusu usajili wa nyota kutoka nje kwa lengo la kuhamasisha ushindani hapa nchini, kwani njia nzuri ya kumpa ujuzi mchezaji ni kumpa nafasi kucheza na yule aliye mzuri zaidi.
“Utamaduni duniani kote, usajili unafanywa na kocha, lakini hapa mchezaji anasajiliwa na mdhamini au kiongozi, mambo ambayo hujiingiza kwenye matatizo, timu ikifungwa wanachama wanakufuata nyumbani. Mi huwa nashangaa timu ikifungwa watu wanavamia viongozi, kumbe hatujajiweka vizuri,” alisema.
Tenga alitaka wataalamu ndio wapewe jukumu hilo, huku akisisitiza kuwa, vijana wenye vipaji ambao wapo hivi sasa hapa nchini wapewe nafasi na si lazima kukimbilia nje, labda iwe kwa mchezaji mzuri zaidi.

Post a Comment

Previous Post Next Post