YANGA KULA SENENE HADI JUMATATU



Kikosi cha Yanga
Kamati ya Ligi imesogeza mbele kwa siku moja mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Kagera Sugar na Yanga iliyokuwa ichezwe kesho (Oktoba 7 mwaka huu) mjini Bukoba kutokana na Uwanja wa Kaitaba kuwa na shughuli nyingine za kijamii. 
Sasa mechi hiyo itachezwa Jumatatu (Oktoba 8 mwaka huu) kwenye uwanja huo huo. Mabadiliko hayo pia yameathiri mechi kati ya Toto Africans na Yanga iliyokuwa ichezwe Oktoba 10 mwaka huu Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Mechi hiyo sasa itachezwa Oktoba 11 mwaka huu.
 

Post a Comment

Previous Post Next Post