ALIYEKUWA Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Davis Mosha ambaye
alijiuzulu wadhifa huo, ametaka kutohusishwa na aina yoyote ya migogoro inayoendelea katika klabu hiyo, kwa kuwa alijiweka
pembeni siku
nyingi.
Akizunguza Dar es Salaam jana, Mosha alisema kwamba
kumekuwa na tetesi kuwa yeye anahusika katika mgogoro unaoendelea hivi
sasa katika klabu hiyo, kitu ambacho kimemshtua yeye pamoja na familia yake na jamaa zake wa karibu.
"Ikumbukwe kuwa mimi
nilishajiondoa kwenye mambo ya mpira nilibakia Yanga kama mwanachama wa
kawaida tu, sasa inashangaza pale ninapoingizwa katika migogoro
ambayo siifahamu kwani hii inaniharibia heshima yangu na hata kwenye
biashara zangu pia," alisema Mosha.
Alisema yeye hakuutuma
uongozi umchezeshe beki wao Nadir Haroub 'Cannavaro' aliyekuwa
akitumikia kadi nyekundu, na hausiki na vipigo ambavyo timu yao ilipata na hivyo kupoteza ubingwa, hivyo ameomba
wafuatwe
wahusika na si yeye ambaye amejikita kwenye biashara zake.
Mosha
alisema anaipenda Yanga lakini kamwe hawezi kujihusisha na kitu chochote
ndani ya klabu hiyo, japo kuna wakati aliwahi kutoa nafasi kwa uongozi kuwa endapo watahitaji msaada wake kifedha waende kwa kuwa
anapenda maendeleo ya timu hiyo.
Alisema ameshaanza kuzungumza na
mwanasheria wake ili kuwachukulia hatua wale wote ambao watakuwa
wanamuhusiha na migogoro ya klabu hiyo kwani kwa kiasi kikubwa
wanaathiri biashara zake, hivyo sheria tachukua mkondo wake kwa wale
wote watakaoendelea kumfuatafuata pasipo kuwa na ushahidi.
huyu mchagga aache kutapatapa,yeye mwenyewe ndio labda anajihusisha na hicho kinachoitwa mgogoro wa yanga lakini hakuna mwenye muda wa kumuhusisha.
ReplyDeletemdau wa bomba,boston,usa