YANGA WAJINOA KWA PENALTI


Kocha mkuu wa Yanga ,Mserbia Kostadic Papic juzi alitoa zoezi la wachezaji wake kupiga pelnati kwa wingi kutokana na kuhofia uenda timu hiyo ikatoka sare ya  bao 1-1 na mshindi akaamuliwa kwa matuta .
Akizungumza  jijini jana , kocha huyo alisema kuwa mara nyingi kikosi hicho kimekuwa kikipata shida sana pindi inapofika wakati wa kupiga pelnati.
Kocha huyo alisema kuwa zoezi hilo lilifanywa na wachezaji wote ambapo wengi wao walikuwa wanashindwa kufanya vile inavyotakiwa .
“Mara nyingi inapofika wakati wa matuta wachezaji wengi ushindwa kufanikisha baoa jambo ambalo linatia shaka”alisema Papic
Kocha huyo alisema kuwa anaisi katika mchezo huo dhidi ya Zamalek timu hiyo zitaweza kutoka sare ya bao 1-1 ndiyo maana ameamua kuendesha zoezi hilo .
Katika mazoezi ya juzi na jana asubuhi  wachezaji waliokuwa wakionyesha uwezo wa kufunga wakati wa upigaji walikuwa ni Nadir Aroub ‘Cannavaro’,Hamis Kiiza, Keneth Asamoah na Devis Mwape.
Katika hatua nyingine msemaji wa klabu hiyo Luis Sendu alisema kuwa upande wa mchezaji Haruna Niyonzima anatarajiwa kutua jijini kesho mapema iliaondoke na kikosi jioni .
Sendeu alisema kuwa lazima mchezaji huyo awasili hapa jijini kwanza ndipo aondoke hata kama akichelewa na kukuta kikosi hicho kimeondoka.
Rwanda hakuna ndege ya moja kwa moja kwenda Misri hivyo lazima Haruna aje hapa nchi hivyo hata kama kikosi kitakuwa kimeondoka basi atapanda ndege ya moja kwa moja kuja Misri”alisema Sendeu



Post a Comment

Previous Post Next Post