Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limemteua Alfred Kisongole Lwiza kuwa Kamishna wa mechi ya Ligi ya Mabingwa (CL) kati
ya El Merreikh ya Sudan na FC
Platinum ya Zimbabwe.
Mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya kwanza itachezwa Aprili 7 mwaka huu kwenye Uwanja wa El Merreikh jijini Khartoum, Sudan kuanzia saa 2 kamili usiku. Katika mechi ya kwanza iliyochezwa
wikiendi hii jijini Harare
timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2.
El Merreikh ni moja ya timu
ambazo CAF iliziingiza moja kwa moja katika raundi ya kwanza. FC Platinum
iliingia raundi ya kwanza baada ya kuing’oa Green Mamba ya Swaziland katika raundi ya awali.
MTIHANI WA MAWAKALA KESHO
Mtihani kwa ajili ya mawakala
wa wachezaji wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika Machi 31 mwaka huu
saa 4 kamili asubuhi ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (FIFA).
Watu watatu wamejitokeza
kufanya mtihani huo utakaokuwa na sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ni maswali
kutoka FIFA wakati nyingine ni kutoka TFF.