Michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ambayo
iko katika mzunguko wa pili inaendelea tena leo (Machi 2 mwaka huu) na kesho
(Machi 3 mwaka huu) baada ya kusimama kwa wiki moja kupisha mechi kati ya timu
ya Taifa (Taifa Stars) dhidi ya Msumbiji (Mambas).
Leo kwenye Uwanja wa Chamazi
jijini Dar es Salaam kutakuwa na mechi kati ya JKT Ruvu na Toto Africans. Mechi
za kesho (Machi 3 mwaka huu) ni kati ya Oljoro itakayokuwa mwenyeji wa Kagera
Sugar kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini
Arusha.
Nayo Polisi Dodoma ikiwa
chini ya makocha Rashid Chama na Henry Mkanwa itakuwa ugenini kwenye mashamba ya
miwa ya Mtibwa mjini Turiani kuikabili Mtibwa Sugar ya huko.
Machi 5 mwaka huu Moro United
inayofundishwa na Hassan Banyai itaoneshana kazi na JKT Ruvu ambayo iko chini ya
Charles Kilinda katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Chamazi jijini Dar es
Salaam.
Mechi za Machi 7 mwaka huu ni
kati ya Oljoro na Toto African (Sheikh Kaluta Amri Abeid), Simba na Kagera Sugar
(Uwanja wa Taifa) wakati Azam itakuwa mwenyeji wa Coastal Union kwenye Uwanja wa
Chamazi.