YANGA WASHTUKIA KOMBE LA URAFIKI NA KUAMUA KUJITOA


KLABU ya soka ya Yanga imetangaza kujitoa kwenye michuano ya kombe la Tanzania ‘Urafiki’ inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho Visiwani Zanzibar.
Michuano hiyo itakayotimua vumbi kwenye Uwanja wa Amaan Visiwani humo ambapo Yanga ilikuwa ifungue kwa kucheza na Jamhuri ya Pemba huku makamu wa kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad akitarajiwa kuwa mgeni rasmi.
Ofisa habari wa Yanga Louis Sendeu alisema kwamba sababu ya kutoshiriki michuano hiyo ni kuhofia kuwa na majeruhi wengi ambao watapelekea kushindwa kutetetea ubingwa wao wa michuano ya Kagame.
Alisema kama waandaaji wa michuano hiyo wangeisogeza mbele wangeweza kushiriki, lakini kwa kuwa zimebaki siku chache kabla ya kuanza kwa michuano ya Kagame itawawia vigumu.
“Tunapenda sana kushiriki michuano ya Urafiki lakini kwa vile itakuwa karibu na Kagame itatuwia vigumu kushiriki kwani tunaweza kujikuta tunamajeruhi wengi na matokeo yake tukashindwa kutetea vema kombe letuy la Kagame,”alisema.

Post a Comment

Previous Post Next Post