TBF NAYO YAWATUPA JELA WACHEZAJI, VIONGOZI


KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), imewafungia baadhi ya wachezaji, viongozi na waamuzi kwa utovu wa nidhamu na ukiukwaji wa taratibu za mashindano.
Katibu Msaidizi wa TBF, Michael Maluwe, amesema utovu huo wa nidhamu ulifanywa na wahusika wakati wa michuano ya Kombe la Taifa, iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana ambapo  Kamati ya Utendaji iliyoketi hivi karibuni jijini Dar es Salaam ilitoa maamuzi hayo baada ya kikao chake cha kupitia ripoti za michuano mbalimbali .
Alisema viongozi watatu wa Mkoa wa Shinyanga  Ibrahimu  Rushemeza, Henry Kizinja William na Tito Nyalalu wamefungia mwaka mmoja kwa lugha za kebehi, vitisho  na matusi  kwa watendaji wa TBF, pamoja na kulazimisha na kushawishi timu zigomee michuano katika vikao halali.
"baada ya mechi viongozi hao walivuruga  taratibu za kikao wakishinikiza kulipwa fedha, hivyo hawataruhusiwa kushiriki au kuongoza timu ndani na nje ya nchi"Alisema.
Alisema, kamati hiyo pia ilijadili hali iliyotokea katika uwanja wa Leaders ya Kocha Msaidizi wa Mkoa wa Mwanza, Amri Mohamed, kutokana na kufanyika vitendo vya utovu wa nidhamu walipocheza na Unguja.
Alisema pamoja na  Mwanza kugomea mechi ya kusaka mshindi wa tatu kwa wanaume, pia ilikaidi adhabu iliyopewa na TBF baada ya kuvunja kanuni za michuano hiyo kuhusu usajili wa wachezaji ambapo waliingiza wachezaji wa timu yao uwanjani wakati wa mchezo wa fainali huku timu mbili husika katika mchezo huo zikijiandaa kukaguliwa.
"Kitendo hicho kiliashiria kuleta vurugu na uharibifu wa amani ya mchezo mbele ya mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, hivyo kuitwa polisi wa ziada kulinda usalama.
Kutokana na vitendo hivyo, mkoa na viongozi wa Mwanza wamefungiwa mwaka mmoja kushiriki michuano yoyote itakayoandaliwa na TBF, huku katika kipindi hiki cha adhabu  viongozi hao hawataruhusiwa kushiriki au kuongoza ama kujishulisha na mpira wa kikapu katika michuano yoyote, kliniki za mpira wa kikapu, michuano ya shule kitaifa, kushiriki mikutano yoyote ya wadau nchini na nje ya nchi.
Kama hiyo haitoshi  adhabu hiyo imekwenda pia kwa wachezaji  Juma Kisoky, Willison Masanja, Shilinde Francis, Amon Sembelya Mohamedi Ally, Amri Mohamedi, Kizito Bahati, Ahmed Said, Adam Jegame, Bundala, Charles, Chacha Tubet, Shinda Vincent, Enock Charles na Kocha Robert Mwita.

Post a Comment

Previous Post Next Post