ETI YANGA HAIJUI ITARUDIANA WAPI NA ZAMALEK


MABINGWA wa soka Tanzania Bara Yanga wamesema bado hawajaelewa mechi yao inachezwa wapi na lini baada ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kushindwa kuleta taarifa kwa wakati.
Yanga inayochea mechi yake ya marudiano na Zalalek ya kuwania Kombe la Klabu Bingwa Afrika ambapo mechi yake ya kwanza ilifanyika nchini Februali 18.
Katibu Mkuu wa Yanga Mwesigwa Selestine, alisema kuwa mpaka jana hawajui wanachezea wapi na tarehe ngapi.
Alisema kisheria taarifa zinatakiwa zifike katika klabu yao kwa muda wa siku kumi kabla ya mechi lakini mpaka sasa kimya.
"Mpaka sasa wala hatuji wapi tunaenda kucheza na ligi...maana hatujaambiwa chochote tunashindwa hata kutafuta kibali (Visa) kwa wachezaji wetu ambao tunataka waende hiyo safari"alisema Mwesigwa.
Alisema wao wamekuwa wakipata taarifa kupitia mtandao hivyo aka hawajui nini wafanye.
Selestine alisema kama wataenda kucheza Misri au nchi yoyote watakayoambiwa wataondoka Alhamis ya Machi mosi kwa kuwa tayari wameshasikia kuwa mechi itacheza Jumamosi.
Akizungumza maandalizi ya mchezo yao Katibu huyo wa Yanga alisema timu yao inaendelea vizuri na mazoezi chini ya kocha Mkuu Kostadin Papic.
Selestine alisema hata mchezaji wao Yaw Berko ambaye alikuwa nje muda mrefu ameanza mazoezi ya kujiandaa na mchezo huo. 
Alisema Berko yupo katika mazoezi ya pamoja na wenzake hivyo maamuzi ya kwenda kwenyemechi yao ni ya kocha wao mkuu Papic ndiye anaweze kusema kuwa anaqweza kucheza au la.
Yanga ilitoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Zamalek hivyo inahitaji ushindi wa ugenini ili iweze kusonga mbele katika mashindano hayo.

Post a Comment

Previous Post Next Post